Habari
Picha: Tamasha la Nyama Choma lafana jijini Dar
Tamasha la Nyama Choma linalohusisha ulaji wa nyama zilizochomwa na wachomaji wa aina mbalimbali kutoka Afrika Mashariki limefanyika jana katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na watu wa rika zote.
Tamasha hilo ambalo limedhaminiwa na Heineken ,Henessy pamoja na JackDaniels lilipambwa na muziki kutoka kwa Mashujaa Band pamoja na michezo ya watoto na wakubwa.
Band ya Mapacha watatu ikiongozwa na Jose Mara
Wadau wakipata moja moto, moja baridi
Mwandaaji wa tamasha la Nyama Choma, Carol Ndosi akihojiwa
Band ya Mapacha watatu ikiongozwa na Jose Mara
Mtoto akionyesha uwezo wake wa kucheza muziki
Wadau wakipata moja moto, moja baridi