Burudani

Tamasha la Tigo Fiesta laacha gumzo jijini Arusha, Whozu apanda stejini na Briefcase lililojaaa mishkaki (Picha)

Jiji la Arusha, jana lilishuhudia show za kufunga mwaka zilizojaa ubunifu na vituko vya aina yake kutoka kwa wasanii mbali mbali waliopanda jukwaani kutumbuiza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyilka katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Msanii Whozu alikuwa ni kivutio kikubwa kutokana na staili aliyotumia kupanda jukwaani na madensa wake wakiwa wamevalia nguo za wapishi huku akiwa na briefcase lililojaa mishkaki.

Mashabiki wengi walipigwa na butwaa baada ya kuona Whozu akifungua briefcase ambalo lilionekana ni la thamani na kutoa mishkati kisha kutuimbuiza na simbo wa Ita Boda boda Twende Kwa Mromboo ambao ulikuwa ni kivutioa Whozu na madensa wake, walifanikiwa kuliteka vyema jukwaa ambapo wakitumbuiza huku wakiwa wanatafuna mishkaki.

Wasanii wengine ambao walifanikiwa kuteka nyoyo za mamia ya mashabiki waliofurika kwenye tamasha la hilo ni pamoja na Roma, Stamina ambao walipanda jukwaani pamoja na mwanadada Maua Sama anayetamba na kibao chake cha Iokote.

Wasanii wengine walipanda sjejini ni pamoja na Dogo janja, Lulu Diva, Rich Mavoko, Fid Q, Weusi na wengine.

Ikiwa ni sehemu ya Vibe la Tigo Fiesta 2018, kampuni ya simu za Simu za mkononi ya Tigo imewaletea promosheni bab-kubwa inayojulikana ya Data Kama Lote inayowapa wateja bonasi ya hadi mara mbili kwa vifurushi vya intaneti watakavyonunua kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*0#.

Tigo pia inatoa punguzo kubwa la bei kwa tiketi za tamasha la Tigo Fiesta 2018 zitakazonunuliwa kupitia Tigo Pesa Masterpass QR. Wateja wanapaswa kupiga *150*01#  na kuchagua 5 (lipia huduma) kisha kuchagua namba 2 (lipa Masterpass QR) na kutuma kiasi husika cha bei ya tiketi kwenda namba ya Tigo Fiesta 78888888.

Wateja wa Tigo pia wanaweza kujaribu umahiri wao wa kujibu maswali yanayohusiana na msimu wote wa vibes kupitia shindano la Tigo Fiesta 2018 – Chemsha Bongo Trivia.  Washindi wanajinyakulia zawadi za kila siku za TSH 100,000, zawadi za wiki za TSH 1 milioni, simu janja za mkononi zenye thamani ya TSH 500,000 kila moja, pamoja na donge nono la TSH milioni 10 kwa mshindi wa jumla.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents