Habari

Tandika: Daladala yagonga treni, wawili wafariki dunia

Watu wawili wamekufa na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika ajali iliyotokea leo asubuhi ikihusisha gari ya abiria aina ya coaster kukigonga kichwa cha treni maeneo ya Yombo Devis Kona.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto amesema watu wawili wamefariki dunia akiwamo mwanamke mmoja na mwanaume mmoja ambaye ni kondakta wa daladala hiyo.

Muroto amesema mbali na watu wawili kufariki pia kuna majeruhi 36 wanne kati yao wakiwa mahututi.

Amesema majeruhi mahututi ni wanawake watatu na mwanaume mmoja.

“Majeruhi wite wanapatiwa matibabu katika hospitali ya Temeke na miongoni mwa majeruhi hao wanne wapo katika hali mbaya”amesema Kamanda Muroto.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents