Michezo

Tanzania kuikabili Libya Jumapili hii

Timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), itashuka dimbani siku ya Jumapili ya Desemba 3 huko nchini Kenya kuikabili Libya katika michuano ya Chalenji mwaka 2017.

Kilimanjaro Stars, ikifanya mazoezi mbalimbali katika Uwanja wa Gymkhana, Dar es Salaam

Kilimanjaro Stars itacheza mchezo huo wa kundi A, katika kuwania kombe la michuano ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA ambayo inatarajiwa kuchezwa nchini Kenya kuanzia Desembe 3 hadi 17 mwaka huu.

Mataifa 10 yanatarajiwa kushiriki katika michuano hiyo mikubwa kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki huku droo ya hatua ya makundi ikionyesha mwenyeji Kenya itacheza mchezo wa ufunguzi dhidi ya Rwanda huku Tanzania ikiikabili Libya siku hiyo.

Kundi A: Kenya, Rwanda, Libya, Tanzania na Zanzibar

Kundi B: Uganda, Zimbabwe, Burundi, Ethiopia na Sudan Kusini.

Michuano hiyo itachezwa katika uwanja wa Bukhungu mjini Kakamega, Afraha Nakuru, Mumias Sports Complex na Moi, mjini Kisumu.

Hata hivyo, kuna wasiwasi michuano hii isifanyika mjinui Kisumu kwa hofu za kiusalama kwa mujibu wa chama cha soka nchini Kenya na sasa uwanja wa Machakos utatumiwa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents