Michezo

Tanzania yafungwa na Brazili hatua ya fainali kombe la Dunia Urusi

Timu ya Wasichana ya Tanzania inayoundwa na Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wa Kituo cha TSC Mwanza wamekubali kipigo cha bao 1 – 0 kutoka kwa Brazili mchezo wa hatua ya fainali ya michuano hiyo ya Kombe la Dunia la Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu  ikiwa chini ya Shirika la Street Child United.

Kwenye mashindano hayo yaliyofikia tamati hii leo kwa kupigwa mechi ya fainali upande wa wanawake na wanaume na mshindi wa tatu.

Tanzania yatinga hatua ya fainali kombe la Dunia Urusi

Mshindi wa tatu kwa wanawake ni Uingereza baada ya kuchomoza na ushindi wa mabao 2 – 0  dhidi ya Ufilipino huku kwa wanaume ni Burundi baada ya kuibwaga Indonezia magoli 3-1.

Bao la dakika za mwisho kwenye kipindi cha kwanza lilitosha kuwapa Brazili ubingwa huo mwaka huu huku Tanzania ikifanikiwa kushika nafasi ya pili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents