Tanzania’s Next Top Model kusakwa
Shindano la kumsaka Mwanamitindo bora wa Tanzania, ‘Tanzania Next Top Model’, lililokuwa lifanyike Novemba 27 sasa limepangwa kufanyika Desemba 3 mwaka huu katika kwenye Ukumbi wa Sweet Easy jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Smilling Faces Caroline Zayumba ambao ndiyo waandaaji wa shindano hilo, alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, kuwa wamesogeza mbele shindano hilo ili washiriki wengi wahudhuria katika mahafali ya kuhitimu elimu zao katika ngazi ya vyuo vikuu, ambako kwa kipindi hicho hawatakuwa katika majukumu hayo.
Carolina aliendelea kusema kuwa kutokana na sababu hiyo iliyotolewa na washiriki wengi, tumeona ni bora kuahirisha shindano hadi katika muda huo uliopangwa.
Baadhi ya washiriki katika shindano hilo, tayari wameishaanza kuchujwa na mmoja wa majaji wa shindano hilo Nafsika Calviaris, kutoka nchini Marekani kutokana na kushindwa kufikia vigezo vinavyohitajika na waandaaji.