Habari
Tanzia: Kapteni John Komba afariki dunia
Habari zilizotufikia kutoka katika vyanzo vya kuaminika zinaeleza kuwa Mbunge wa Mbinga kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mh. John Komba amefariki.
Kapteni Komba amefariki leo (Februari 28, 2015) majira ya saa kumi jioni katika hospitali ya TMJ, Dar es Salaam.
Tutaendelea kukupatia taarifa zaidi kadri tutakavyokuwa tunazipata.
Bongo 5 inawapa pole familia ya marehemu na wote walioguswa na msiba huu.