Habari
TANZIA: Mbunge Ngonyani (Profesa Majimarefu) afariki dunia
Mbunge wa Korogwe vijijini (CCM), Stephen Ngonyani (Profesa Maji Marefu) amefariki dunia usiku huu katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa wateja wa Muhimbili, Aminiel Aligaesha amethibitisha.
June 6, 2018 Mbunge huyo alifiwa na mke wake, Mariam aliyekuwa akipatiwa matibabu hospitali ya Taifa Muhimbili.