Habari
TANZIA: Mbunifu wa filamu za Spider-Man, the X-Men, Iron Man, Black Panther, The Incredible Hulk na the Fantastic Four afariki dunia
Mkongwe wa maswala ya uwandishi wa vitabu vya ‘Caton’ maarufu kama ‘Comics’ na mbunifu wa filamu za Spider-Man, the X-Men, Thor, Iron Man, Black Panther, Silver Surfer, The Incredible Hulk na the Fantastic Four, anayejulikana kwa jina la Stan Lee amefariki dunia.
Lee aliyeanza kazi hiyo kuanzia mwaka 1939 na kubuni Black Panther, Spider-Man, the X-Men, the Mighty Thor, Iron Man, the Fantastic Four, the Incredible Hulk, Daredevil na Ant-Man, zenyestori nzuri zinazoendana uhalisia wa maisha ya kawaida amefariki dunia hapo jana siku ya Jumatatu huko Cedars-Sinai Medical Center jijini Los Angeles na familia yake kumwambia mwandishi waHollywood.