Michezo

TANZIA: Ndikumana afariki dunia ghafla baada ya mazoezi

Mchezaji wa timu ya taifa ya Rwanda na beki wa zamani wa klabu ya Rayon Sports ya Rwanda, Ndikumana Hamad Katauti amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuanguka ghafla.

 

Taarifa kutoka Kigali, Rwanda zinaeleza kuwa Hamad Kataut kabla ya kufikwa na umauti alikuwa mazoezini jana asubuhi.

Katauti alikuwa kocha msaidizi wa kikosi cha Rayon Sports ya Rwanda, enzi za uhai wake na aliwahi kuichezea klabu ya Stand United ya Shinyanga akitokea timu ya Cyprus.

Ndikumana alikuja nchini siku ya Simba Day Agosti 8 mwaka huu akiwa na kikosi cha Rayon ambacho kilicheza na Simba na kufungwa bao 1-0.

Mchezaji Ndikumana Hamad amewahi kuwa mume wa muigizaji filam maarufu nchini, Irene Uwoya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents