Burudani
Tanzia: Rapper Pink afiwa na mama yake mzazi
Rapper Pink amepata pigo la msiba mzito kwa kufiwa na mama yake mzazi Jumamosi hii.
Akiongea na Bongo5, mtayarishaji wa muziki nchini Mbezi, ambaye pia anamsimamia msanii huyo amesema kuwa marehemu amefariki baada ya kulazwa hospitalini kwa siku mbili.
“Marehemu alilazwa for two days ya tatu leo [Jumamosi] ndio akafariki katika hospitali ya Amana majira ya saa 12 na nusu jioni. Alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Pneumonia,” amesema.
Bongo5 tunatoa pole kwa msiba huo lakini pia endelea kutufuatilia kwa ajili ya kupata taarifa zaidi za msiba huo.