Michezo

TASWA yapongeza wanawake wa gofu

CHAMA cha waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) kimetoa pungezi kwa  kwa timu ya  gofu ya Taifa ya wanawake ambayo mwisho mwa wiki ilitoa kimasomaso na kuweka historia  katika michuano ya gofu ya wanawake  kombe la  Challenge Afrika baada ya kufanya vizuri na kushika nafasi ya pili  kwenye michuano hiyo iliyofanyikia katika viwanja vya  Klabu ya IBB International mjini Abuja.

Amiri Mhando,Katibu mkuu wa TASWA alisema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na kusema, Tanzania  ilishika nafasi ya pili kati ya nchii 4 baaada ya kukusanya mikwaju  ya 472 katika ya raundi  ya tatu za viwanja vya IBB  vyenye par 74 huka Afrika ya Kusini  ilitetea taji hilo na kuibuka bingwa  katika mchezo huo kwa kupata mikwaju 440  huku Zimbabwe ijinyakulia nafasi ya tatu kwa kupata mikwaji 475  na ikifwatiwa na Zambia iliyopata mikwaju 485.

Tunaseama tunawapongeza timu ya wanawake na wadau wengine wote waliowawezesha  kwani ni mara ya kwanza timu ya gofu ya wanawake kufanya vizuri , hasa tukikumbuka  michuano  iliyofanyika  Cairo mwaka 2008 Tanzania  ilishika nafasi ya 8.

‘Taswa tumefurahishwa sana na pia tunawaomba wachezaji wa gofu waliotoka Abuja ambao ni Hawa Wanyeche Madina, Iddi na pamoja na Shazi Myombe, wasibwete  na kujisahau  bali waongeze juhudi na kuzidi kuitangaza nchi,’ alisema Mhando.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents