Michezo

Tazama magari ya kifahari anayomiliki Aubameyang, thamani yake sio mchezo

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang ameonekana kuwa na mapenzi makubwa ya kumiliki magari ya kifahari.

Miongoni mwa magari hayo ya kifahari ambayo anamiliki mchezaji huyo ni pamoja na Porsche Panamera Turbo Techart ambalo thamani yake ni paundi 140,000 ambapo kwa fedha za kitanzania ni zaidi ya milioni 442.


Porsche Panamera Turbo Techart

Lamborghini Aventador ambalo thamani yake ni paundi 270,000 sawa na zaidi ya milioni 853 kwa fedha za kitanzania na Ferrari 812 Superfast ambayo ina gharimu paundi 250,000 (zaid ya milioni 790).


Lamborghini Aventador

Ndinga nyingine ya kifahari ambayo anamiliki Aubameyang ni Range Rover Sport Mansory ambayo thamani yake ni paundi 150,000, ni zaidi ya shilingi milioni 474 kwa fedha za kitanzania.


Ferrari 812 Superfast


Range Rover Sport Mansory

Magari mengine ambayo anamiliki Aubameyang ni:

Audi R8 V10 Plus – £128,000

Aston Martin DB9 Volante 2 – £140,000

Ferrari 488 Spider – £205,000

Porsche Panamera Mansory C One – £113,000

Volkswagen Beetle Cabriolet – £22,000

Porsche Cayenne Techart Magnum – £60,000

Ferrari 458 Italia – £200,000

Audi R8 2013 – £128,000

Lamborghini Gallardo LP560-4 – £141,000

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents