Habari
Tazama muonekano wa nje na ndani wa jumba la kifahari la Rais Mugabe ambako amezuiliwa na jeshi (+Picha)
Wakati nchi yake ikiwa kwenye orodha ya nchi masikini duniani lakini hiyo ni tofauti kabisa na maisha ya kiongozi wao, Robert Mugabe ambaye wiki hii jeshi la nchi hiyo limemshikilia nyumbani kwake kwa sababu za kiusalama.
Rais Mugabe ambaye ameitawala Zimbabwe kwa miaka 37 katika kipindi chote hicho nchi hiyo imetajwa kuwa kwenye mtikisiko mkubwa wa kiuchumi na kisiasa.
Hapa zimenyakwa picha za jumba lake la kifahari lililopo katika eneo la Borrowdale jijini Harare lenye vyumba 25 vya kulala, Swimming Pool tatu na Sebule 5. Na jumba hili ndio sehemu ambayo Rais Mugabe ameshikiliwa kwa muda na Jeshi la nchi hiyo.