Tazama picha za warembo 20 watakaowania taji la Miss Rwanda 2018
Jana usiku wa kuamkia leo Jumapili Februari 4, 2018, kulikuwa na mchujo wa kuwapata warembo 20 ambao watafuzu katika hatua za mchujo wa kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha Miss Rwanda 2018.
Ikiwa ni tofauti kidogo na Tanzania katika hatua za mchujo, Warembo hao walianza kwa kuulizwa maswali na jopo la majaji ambapo kulikuwa na wasichana 35 walioshinda kutoka kwenye mikoa mbalimbali nchini humo hadi kupata washiriki 20.
Jopo hilola Majaji limeundwa na majaji watatu ambao ni pamoja na Miss Rwanda namba mbili mwaka 2009 Rusaro Carine, Mtangazaji wa Kiss FM Sandrine Isheja Butera na Francine Uwera Havugimana kutoka shirikisho la taasisi binafsi.
Matokeo ya ushindi wa warembo hao yamepatikana kwa kuangalia urembo (maksi 30), majibu ya maswali waliyoulizwa (maksi 40) na ustadi wa kujibu maswali (maksi 30) na kilele cha mashindano hayo ni Tarehe 24 Februari, 2018 na sherehe zitafanyika katika ukumbi wa Kigali Convention Centre.
Tazama picha za warembo hao na majina yao;
Picha kwa hisani ya Mtandao wa Inyarwanda