Burudani

Temba apandishwa mahakamani kwa kutishia kuua

Msanii kutoka TMK Wanaume Family, Amani James aka Mh Temba jana amefikishwa katika mahakama ya mwanzo ya Temeke jijini Dar es salaam akikabiliwa na mashitaka ya kutishia kuua kwa kisu kutokana na wivu wa mapenzi.

Temba kutoka TMK akiimba na  mashabiki wa muziki wa Mtwara katika serengeti fiesta 2013.

Kwa mujibu wa Nipashe, Temba alipandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake mbele ya hakimu Claudia Frank wa mahakama hiyo.
Mheshimiwa Temba alifikishwa mahakani hapo mapema saa 3:00 asubuhi huku akiwa amefungwa pingu chi ya ulinzi wa askari kanzu wa kituo cha Mkoa wa Kipolisi Chang’ombe.

Aliwekwa chini ya ulinzi katika kituo cha mahabusu ya mahakama hiyo kabla ya kusomewa mashitaka yake. Kesi hiyo imesajiliwa mahakamani hapo kwa namba 371 chini ya kifungu cha 89 kidogo cha (2) (a) sura ya 16 ya mwenendo wa sheria ya Makosa ya Jinai.

Akisomewa mashitaka na karani wa mahakama hiyo, Joyce Ngamesha, alidaiwa kuwa Januari 28, mwaka huu, saa 1:00 jioni katika baa ya Scorpion Iiliyopo Temeke jijini Dae es salaam, mshitakiwa alimtishia kumchoma kisu Godrey Deogratius ama Sulla.

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo na yupo nje kwa dhamana.

Hakimu Frank alisema kesi hiyo itasikiliza ushahidi March 11, mwaka huu,. Kabla ya kufikishwa mahakamani hapo, Mshitakiwa alifikishwa katika kituo cha polisi cha Chang’ombe akituhumiwa kutishia kumchoma kisu mlalamikaji kwa madai ya kuwa na mahusiano wa kimapenzi na mke wa msanii huyo.

Ilidaiwa kuwa mshitakiwa alimtishia kumchoma kisu mlalamikaji huku akijua ni kinyume na sheria.

Source:Nipashe

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents