TETESI: Kylian Mbappe kutua Madrid, wengine wanaotikisa soko la mwezi Januari hawa hapa
Mshambuliaji wa klabu ya Paris St-Germain na timu ya taifa ya Ufaransa, Paris St-Germain anawaniwa kwa karibu mno na mabingwa wa kihistoria wa Champions League timu ya Real Madrid. (Le Parisien – in French)
Borussia Dortmund wako tayari kupokea ofa kutoka kwa winga wa England, Jadon Sancho, mwenye umri wa miaka 19, mapema Januari. (The Independent)
Mchezaji wa zamani wa timu ya vijana wadogo ya Manchester City Sancho ndiye anayekosekana katika kikosi cha mashambulizi ambacho kitayafanya mashambulizi ya Liverpool ya kuogopwa zaidi kuliko kilivyo hata sasa, kwa mujibu wa mlinzi wa zamani wa Reds defender Jamie Carragher. (Daily Star)
Manchester United wameachana na mpango wao wa kumchukua mshambuliaji wa Juventus Mario Mandzukic, mwenye umri wa miaka 33 -rais wa Croasia (The Athletic, via Inside Futbol)
Borussia Dortmund wanamlenga Mandzukic pamoja na kiungo wa kati wa Juventus na Ujerumani Emre Can,25, Januari. (Sun)
Bruno Fernandes anayelengwa na Tottenham bado yuko makini kuondoka Sporting Lisbon, licha ya kusini mkataba mpya wa kipengele cha malipo ya pauni milioni 85. Kuna makubaliano yanayomruhusu kiungo huyo wa kati mwenye umri wa miaka 25 kutoka Ureno kuondoka iwapo malipo ya pauni milioni 60 yatapatikana (Mail)Kylian Mbappe (kushoto) atajiunga na Real Madrid
Milan bado iko makini kusiani mkataba na difenda Mturuki Merih Demiral, mwenye umri wa miaka 21, ambae amekuwa akihusishwa na Manchester City pamoja na Arsenal. (Calciomercato)
Arsenal wanapanga kumlipa kiungo wa kati wa Real Madrid Mcolombia James Rodriguez pauni milioni 35 mwenye umri wa miaka 28, ambaye amekuwa akiaminiwa kuwa angependelea kuhamia katika Inter Milan au Paris St-Germain. (Eldesmarque – in Spanish)