Michezo

TETESI: Man United kumuongezea mkataba mrefu zaidi De Gea, kumpatia mshahara wa kufa mtu

Klabu ya soka ya Manchester United hawana mpango kabisa ya kumuachia David de Gea kwenda Real Madrid.

Man United inampango wa kumuongeze mkataba wa miaka mitano mchezaji huyo na kumlipa mshahara wa paundi 350,000 kwa wiki kabla ya kuanza kwa kombe la dunia, hiyo ni kwa mujibu wa gazeti la The Sun.

De Gea ambaye alitua United mwaka 2011 akitokea Atletico Madrid, anatarajia kumaliza mkataba wake mwaka 2019.

Golikipa huyo amekuwa tegemezi katika kikosi cha Man United huku katika msimu huu akiwa anaongoza katika ligi kuu ya Uingereza kwa kuwa na clean Sheet 16 akifuatiwa na golikipa wa Manchester City, Ederson mwenye clean sheet 14.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents