Tetesi za soka barani Ulaya Alhamisi hii, Atletico Madrid yaeleza hatma ya Griezma, Mkurugenzi wa Juventus amfuata Maurizio Sarri London
Mkurugenzi mtendaji wa Atletico Madrid -Miguel Angel Gil Marin amethibitisha kuwa mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, mwenye umri wa miaka 28, atahamia Barcelona msimu huu. (Sport)
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amepuuzilia mbali madai kuwa anaangalia uwekano wa kwenda mapumzikoni mwishoni mwa msimu ujao.(Independent)
Mkurugenzi wa masuala ya mchezo wa Juventus Fabio Paratici amewasili jijini London kukamilisha mkataba kwa ajili ya Meneja wa Chelsea Muitaliano Maurizio Sarri. (Calciomercato)
Lakini Chelsea watakataa kuondoka kwa Sarri hadi washindi hao wa ligi ya Utaliano watakapokamilisha madai ya malipo ya fidia ya Blues. (Mail)
Hatimae Manchester United wamesitisha haja yao ya kumnunua mchezaji wa kimataifa wa Wales Gareth Bale – na kuamua kutomuhamisha winga huyo wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 29. (Evening Standard)Wakala wa Matthijs de Ligt Mino Raiola amekutana na Mkurugenzi wa mchezo wa Paris St-Germain Antero Henrique kuzungumzia juu ya uhamisho wake
Wakala wa Matthijs de Ligt Mino Raiola amekutana na Mkurugenzi wa mchezo wa Paris St-Germain Antero Henrique kuzungumzia juu ya uhamisho wa mchezaji huyo wa safu ya ulinzi ya Ajax na Uholanzi mwenye umri wa miaka 19 . Klabu zote zinakaribia kufikia mapatano ya euro milioni 75. (RMC Sport – in French)
Washindi wa Ufaransa PSG wamemtaka De Ligt asaini nao mkataba wa miaka mitano wa thamani ya euro milioni 12 kwa mwaka. (ESPN)