Michezo

Tetesi za soka barani Ulaya, Barcelona kumng’oa beki huyu wa Man United, Madrid kuvunja rekodi ya usajili kwa Pogba

Barcelona inamnyatia beki wa Manchester United na raia wa Sweden Victor Lindelof, 24, huku ikiwa beki wa Ajax Matthijs de Ligt anatarajiwa kujiunga na Juventus. (Mundo Deportivo – in Spanish)
Victor Lindelof

Real Madrid watalazimika kulipa dau litakalovunja rekodi la £162m kumsaini kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba, 26, kutoka Manchester United. (Marca)Pogba

Mkufunzi wa klabu ya Sheffield Wednesday Steve Bruce ataunga mkono ofa yoyote kutoka Newcastle baada ya kupigiwa upatu kumrithi Rafael Benitez. (Chronicle)

Naibu mkufunzi wa klabu ya Manchester City Mikel Arteta na mkufunzi wa Nice Patrick Vieira wameonywa kuhusu kazi ya Newvcastle na Benitez. (Sun)

Everton ni miongoni mwa klabu zilizo na hamu ya kumsaini kiungo wa kati wa Manchester City na Uingereza Fabian Delph, 29. (Sky Sports)Lukaku

Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anataka mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, kutokubali uhamisho wa kuelekea Inter Milan na badala yake kusalia katika uwanja wa Old Trafford next season. (Sun)

Arsenal wamepatiwa ofa ya kumsaini mshambuliaji wa Real Madrid na raia wa Dominican Republic Mariano Diaz, 25, kwa dau la chini la £18m. (Star)

Everton ina hamu ya kumsaini mshambuliaji kinda mwenye umri wa miaka 19- wa Itali Moise Kean, ambaye klabu yake ya Juventus inataka dau la £31m na kifungu cha kumnunua tena katika makubaliano yoyote. (Mail)Moise Keane

Fenerbahce inataka kumsaini mchezaji wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 30 Mesut Ozil kwa mkopo kutoka Arsenal. (Sky Sports)

Manchester United imewasiliana na Southampton kutaka kujua kuhusu juwepo wa kiungo wa kati wa Gabon mwenye umri wa miaka 25 Mario Lemina. (Sky Sports)

Bournemouth wamempatia kandarasi mpya ya miaka mitano mshambuliaji wa Uingereza Callum Wilson huku West Ham, Chelsea na Everton zikihusishwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27(Sun)Divock Origi

Liverpool wana matumaini kwamba mshambuyliaji wa Ubelgiji Divock Origi, 24, atatia saini ya kandarasi mpya Anfield. (ESPN)

Crystal Palace inakaribia kumsaini kwa mkataba wa kudumu mshambuliaji wa Swansea na Ghana Jordan Ayew, 27, ambaye alihudumu msimu uliopita akiwa kwa mkopo. (Sky Sports)

Mpango a West Ham kumsaini mshambuliaji wa Celta Vigo Maxi Gomez umefutiliwa mbali baada ya klabu hiyo kufeli kukubaliana kuhusu mpango wa malipo wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 raia wa Uruguay.. (Sky Sports)Mario BalotelliHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

The Hammers wamepatiwa ofa ya mshambuliaji wa Marseille Mario Balotelli, 28, kwa uhamisho wa bila malipo kama mbadala wa Wilson na Gomez. (Mirror)

Barcelona wana hamu ya kumsaini mshambuliaji wa Romania Ianis Hagi, mwanawe mchezaji wa zamani wa Barcelona Georghe Hagi, kutoka klabu ya Viitorul Constanta na kumtoa kwa mkopo kwa klabu ya Real Valladolid. (AS – in Spanish)

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents