Michezo

Tetesi za soka barani Ulaya Ijumaa hii, Man United kutumia fedha za Lukaku usajili ujao,  Sanchez na wengine sokoni

Manchester United itakabiliwa na deni la mshahara la pauni milioni 12 kwa mchezaji Alexis Sanchez hata kama atasajiliwa na klabu ya Inter Milan. (ESPN)

Alexis Sanchez

Sanchez, 30, ambaye ni raia wa Colombia alikosa mazoezi ya Alhamisi na klabu yake ya Man United baada ya kwenda ubalozi wa Marekani jijini London. (Sun)

Mshambuliaji wa Ubelgiji Christian Benteke, 28, na mlinzi raia wa England James Tomkins, 30, wapo katika mazungumzo ya kuongeza mikataba yao na klabu ya Crystal Palace. (Guardian)

Barcelona wamekataa ofa ya klabu ya Inter Milan ambao wanataka kumsajili kiungo wa kimataifa wa Chile Arturo Vidal, 32, kwa mkopo. (Mundo Deportivo)Arturo Vidal

Arturo Vidal

Man United wapo ukingoni kukubali mapatano ya kumsajili mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Tottenham na Uhispania Fernando Llorente, 34. (Gazzetta dello Sport – via Star)

Lille wanaamini kuwa watafanikiwa kumng’oa kiungo Mreno Renato Sanches, 22, kutoka Bayern Munich. (L’Equipe)Ole Gunnar Solskjaer

Kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer ataweza kutumia kitita cha pauni milioni 75 kwenye dirisha la usajili la mwezi Januari. Fedha hizo United walizipata baada ya kumuuza mshambuliaji raia wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 26, katika klabu ya Inter Milan mwanzoni mwa mwezi huu. (Talksport)

Kiungo Mreno wa klabu ya Leicester City Adrien Silva, 30, amesafiri kuelekea Monaco kwa ajili ya vipimo vya kiafya vitakavyofanyika leo Ijumaa. Silva anatarajiwa kujiunga na Monaco kwa mkopo. (Daily Telegraph)Willy Caballero

Willy Caballero

Kipa wa Chelsea Muargentina Willy Caballero, 37, anatakiwa na klabu Real Madrid. (Marca – in Spanish)

Ujumbe wa wawakilishi wa Real Madrid upo Ufaransa kufanya majadiliano juu ya uhamisho wa mshambuliaji wa Brazil Neymar, 27 kutoka klabu ya Paris St-Germain. (Marca – in Spanish)Neymar

Miamba ya Uhispania klabu za Real Madrid na Barcelona zinagombea saini ya Neymar kumng’oa PSG.

Winga raia wa Brazil anayekipiga na klabu ya Chelsea Kenedy, 23, anaangalia uwezekano wa kuihama moja kwa moja klabu hiyo kabla ya dirisha la usajili la ulaya kufungwa wiki ijayo. (Goal)

Miamba ya Uturuki klabu ya Fenerbahce imejitenga na harakati za uhamisho wa beki wa Manchester United na Argentina Marcos Rojo, 29. (Star)Marcus Rojo

Fenerbahce wanasema hawataki tena kumsajiri mlinzi Rojo (katikati) kutoka Man United

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents