Tetesi za soka barani Ulaya Jumamosi hii, Inter kumsajili Lukaku, Madrid kuanza na Pogba kisha kumalizana na Eriksen
Inter Milan wanataka kumsaini mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku, 26, lakini watalazimika kumuuza mshambuliaji wao wa sasa Muargentina Mauro Icardi,26 kufadhili mkataba wa Lukaku. (Guardian)
Real Madrid wanampango wa kumnunua Paul Pogba kutoka Manchester United msimu huu wa joto kabla ya kumsaini mchezaji nyota wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen, 27. (Goal)
Tottenham watamchukua winga wa Uhispania wa miaka 22 Marco Asensio kama sehemu ya makubaliano ya uhamisho wa Eriksen kwenda Madrid . (Sun)
Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameiambia klabu hiyo imuuza Pogba kwa klabu itakayoweka dau kubwa zaidi, japo Juventus wameonesha nia ya kutaka kumnunua. (Star)Haki miliki ya pichaREUTERS
Tottenham inatarajia Juventus itaweka dau la kumnunua beki wa kulia Kieran Trippier, 28, na wako tayari kumuuza kiungo huyo wa kimataifa kwa karibupauni milioni 25. (Telegraph)
Paris St-Germain wameiambia Barcelona kuwa hawamuuzi Neymar, 27 kwa udi na uvumba. (Mail)
Real Madrid wanampango wa kusaini Ian Kylian Mbappe,26 kutoka PSG msimu ujao lakini wanataka mchezaji huyo raia wa Ufaransa kutoa ombi la kutaka uhamisho. (AS)Haki miliki ya pichaREUTERS
Atletico Madrid wanamtaka beki wa Arsenal Mhispania Hector Bellerin, 24, na wako tayari kumwachilia winga Vitolo, 29, kama sehemu ya mkataba wa usajili wake. (Telegraph)
Chelsea hawajaamua kumuuza mlinzi wao Mfaransa Kurt Zouma, 24, kwa Everton hadi watakapopata kocha mpya. (Star)
The Blues wanajiandaa kuilipa Derby pauni milioni 4 zinazohitajika kutimiza masharti ya mkataba wa Frank Lampard kabla hawajakamilisha mchakato wa kumuajiri kama kocha wao mpya wiki ijayo. (ESPN)
Chelsea wamempatia kipa Petr Cech la kiufundi na mshauri wa michezo wakiwa na matumaini kuwa atashirikiana kwa karibu na Lampard. (Guardian)Haki miliki ya pichaAFP
Klabu ya Shanghai Greenland Shenhua kutoka China imetoa ofa ya pauni milioni 17.8 kumnunua Willian, 30, lakini mchezaji huyo wa Brazil huenda asikubali kujiunga nao kwasababu bado anataka kusalia Chelsea. (UOL Esporte, via Metro)
Mpango wa Arsenal wa kumnunua winga wa Ubelgiji Yannick Carrasco au mshambuliaji wa Bournemouth Ryan na Uskochi Fraser huenda umekwama. (Evening Standard)
Meneja mpya wa Juventus Maurizio Sarri amesema hana mpango wa kumsaini kiungo wa kati wa Italia Jorginho, 27, kutoka Chelsea. (Sun)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Tetesi Bora Ijumaa
Juhudi za kocha Ole Gunnar Solskjaer kuimarisha kikosi chake huenda zikagonga mwamba kwa sababu Manchester United ni klabu ambayo hutoa ofa ya chini kwa wachezaji wanaotaka kuwasajili. (Evening Standard)
Solskjaer anataka kumuuza kiungo wa kati wa Man Utd Mfaransa Paul Pogba, 26, bada ya kufahamishwa kuwa ana pauni milioni 100 ya kuwasajili wachezaji wapya msimu huu. (Star)Haki miliki ya pichaREUTERS
Mchezaji nyota wa kimataifa wa Brazil Neymar, 27, hana mpango wa kuchezea tena Paris St-Germain. (Sport – in Spanish)
Real Madrid wameweka dau la euro milioni 130 kumnunua Neymar, kutoka PSG, mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 29, au mshambuliaji wa Colombia James Rodriguez, 27. (Mundo Deportivo – in Spanish)
Manchester City wanapigiwa upatu kuipiku Man Utd katika usajili wa Harry Maguire, 26, kutoka Leicester kwa kima cha pauni milioni 65 baada ya kiungo huyo wa England kupita vipimo vya matibabu. (Star)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Kiungo wa kati wa Atletico Madrid Mhispania Rodri, ameamua kujiunga na Man City badala ya Bayern Munich na kuhamia City kawa malipo ua £62m. (Kicker – in German)
Everton wameanza maungumzo na Chelsea kuhusu usajili wa Kurt Zouma kwa mkataba wa kudumu baada ya mlinzi huyo wa Ufaransa, 24, kucheza Goodison Park msimu uliopita kwa mkopo katika. (Telegraph)