Michezo

Tetesi za soka barani Ulaya Jumanne hii, Sergio Ramos amshauri Pogba kuhamia Madrid, Eriksen wengine sokoni

Juventus imekataa kumuuza winga Douglas Costa 28 licha ya Man United kuwa na hamu ya kumsajili baada ya mkufunzi Maurizio Sarri kuzuia uhamisho wa nchezaji huyo wa Brazil. (Mail)

Douglas Costa

Real Madrid itawasilisha ombi la kumsaini kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen msimu ujao iwapo Paul Pogba ataongeza kandarasi yake na Man United .

Eriksen mwenye umri wa miaka 27 atapatikana kwa uhamisho wa bila malipo kwa kuwa kandarasi yake inakamilika 2020. (Sky Sports)

Paul Pogba

Beki wa Real Madrid Sergio Ramos amemshauri Pogba, 26, kutoka Man United na kuhamia katika klabu hiyo ya Uhispania. (Express)

Chelsea imeanzisha mazungumzo na beki wa Itali Emerson, 25, kuhusu kandarasi mpya mpya. Winga wa England Callum Hudson Odoi 18 anakaribia kukamilisha mkataba mpya wa malipo ya £180, 000 kwa wiki katika mkataba wa miaka mitano.. (Express)Hudson Odoi

Tottenham iliwatuma wawakilishi ili kumtazama mshambuliaji wa Fenerbahce Vedat Muriqi, 25, akiichezea Kosovo wikendi iliopita.

Maskauti kutoka Lazio, Fiorentina na Napoli pia walikuwepo huku Muriqi akifunga katika ushindi wa Kosovo wa 2-1 dhidi ya Czech Republic. (Sabah, via Four Four Two)

Mlinda lango wa Manchester United David de Gea, 28, anakaribia kutia kandarasi mpya ambayo itampatia mshahara wa £290,000 kwa wiki ikiwa ni mshahaha anaolipwa Pogba. (Guardian)

Mchezaji wa timu ya Itali ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 Paolo Nicolato amemwambia mshambuliaji wa Everton Moise Kean kujifunza kutokana na makosa baada ya kuwasili kuchelewa katika mkutano wa timu kabla ya mechi dhidi ya Ubelgiji.Mise Kean wa Everton

Kean 19 aliwachwa nje kutoka katika kikosi cha Itali katika mechi za kimataifa za hivi karibuni (Gazzetta Dello Sport, via Sport Witness)

Tottenham ilitaka kumsaini kiungo wa kati wa Roma Nicolo Zaniolo, 20, kulingana na ajenti wa mchezaji huyo kabla ya kumsaini Giovani lo Celso kwa mkopo badala yake. (Mail)

Wolves ilifeli kumsaini kiungo wa kati Leeds Kalvin Phillips msimu huu ,ilibainika baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kutia kandarasi mkataba mpya katika klabu hiyo.. (Football Insider)Giovani lo Celso

Chelsea imeambia maajenti wake wakuu kwamba inaamini kwamba marufuku ya uhaimsho waliowekewa inayowazuia kununua wachezaji msimu huu itapunguzwa , ikimaanisha kwamba wanaweza kununua wachezaji katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari.. (Mirror)

Kiungo wa kati wa Newcastle Jonjo Shelvey, 27, ametaja baadhi ya ukosoaji dhidi Steve Bruce na klabu hiyo kama upuzi na aibu. (Chronicle)Steve Bruce wa Newcastle

Klabu ya ligi ya Bundelsiga Paderborn huenda inataka kufanya jaribio la pili la kumsaini kiungo wa kati wa Crystal Palace Jairo Riedewald, 23, mnamo mwezi Januari baada ya kukosa uhamisho wa mkopo msimu huu . (Football.London)

Beki Jesus Vallejo, 22, aliyejiunga na Wolves kwa mkopo katika dirisha la uhamisho la msimu huu anaweza kuuzwa na klabu ya Real Madrid msimu ujao. (Birmingham Mail)

Tamasha kwa jina A Cirque du Soleil kuhusu mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi liitaanza katika mji wa Catalan mwezi Oktoba. (Standard)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents