Michezo

Tetesi za usajili Alhamisi hii, Pogba, Bale, Mata, Saul, Hazard na wengine sokoni

Uhusiano kati ya Paul Pogba na meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer umeanza kuzorota, kiungo huyo wa miaka 26 huenda akahamia Real Madrid. (Le Parisien via AS)

United inapania kumsajili kiungo wa kati wa Sporting Lisbon na Ureno Bruno Fernandes, 24. (A Bola – in Portuguese)

Gareth Bale, 29, hayupo katika mpango wa Real Madrid msimu ujao, kuna tetesi kuwa klabu hiyo ya Uhispania itamruhusu kuchagua kalbu anayotaka kuhamia.

Tayari Manchester United na Bayern Munich wameonesha nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo. (AS)

Gareth Bale
Image captionGareth Bale (Kushoto)

Kiungo wa kati wa Manchester United Juan Mata, 30, bado hajafanya uamuzi kuhusu hatma ya yake ya siku zijazo Old Trafford.

Mchezaji huyo raia wa Uhispania tayari amepata ofa kutoka kwa vilabu kadhaa. (Manchester Evening News)

Manchester City, Manchester United na Barcelona zinapania kumsajili kiungo wa kimataifa wa Uhispania Saul Niguez, 24. (Mirror)

Mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard, 28, anaamini kuwa uhamisho wake kwenda Real Madrid ni ”sasa la sivyo aachane na mpango huu” . (Goal)

Eden Hazard
Image captionEden Hazard, mshambuliaji wa Chelsea na Ubelgiji

Kiungo wa kati wa Uingereza Danny Drinkwater, 29, ameambiwa hana maisha Stamford Bridge chini ya ukufunzi wa Maurizio Sarri. (Guardian)

Liverpool inatafakari uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Ajax Mbrazili David Neres, 22, huku mahasimu wao wakimnyatia kiungo huyo. (Mirror)

West Ham inaonngoza katika kinyang’anyiro cha kumsajili beki wa kulia na kushoto wa Liverpool Nathaniel Clyne, 28, ambaye kwa sasa yuko Bournemouth kwa mkopo. (Football Insider)

Nathaniel Clyne
Image captionNathaniel Clyne( Kushoto)

West Brom iko tayari kushauriana na meneja wa Preston Alex Neil kuwa meneja wao mpya. (Telegraph)

Kiungo wa kati wa Chelsea Mnigeria Kenneth Omeruo, 25, anataka kugeuza mkataba wake wa mkopo Leganes kuwa wa kudumu kabla ya mwisho wa msimu huu . (Brila)Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anataka kumsajili mshambuliaji mkali kama Jamie Vardy, 32 atakaetoa ushindani mkali kwa washindani wao. (Leicester Mercury)

Chanzo BBC.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents