Michezo

Tetesi za usajili barani Ulaya Jumatano hii, Mourinho, Klopp, Bale, De Ligt, Werner na wengine sokoni

Meneja wa zamani wa Manchester United Jose Mourinho anakaribia kuwa tayari kwa asilimia 100% kurejea katika klabu ya Real Madrid msimu huu ,baada ya kuiacha na kujiunga tena na Chelsea mwaka 2013. (Telegraph)

Rais wa Real Florentino Perez anaangalia uwezekano wa kumfuta kazi meneja Santiago Solari mara moja baada ya timu hiyo ya Ligi ya Championi kufungwa na Ajax Jumanne, lakini anahisi kwamba hakuna uwezo wa kuongoza kwa kipindi kilichobaki cha msimu. (Marca)

Perez alifanya mazungumzo ya dharura na wakurugenzi wa klabu katika mji wa Bernabeu hadi 02:00 baada ya kushindwa. (AS)


Winga wa Wales Gareth Bale, mwenye umri wa miaka 29, anaweza kupoteza kiasi cha pauni milioni sabini (£70m), ikiwa atahamia Real Madrid

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atakataa pendekezo lolote kutoka kwa Real la kumchukua to Bernabeu msimu huu . (Telegraph)

Winga wa Wales Gareth Bale, 29, anaweza kupoteza kiasi cha pauni milioni sabini (£70m) za mshahara wake ikiwa ataondoka Real msimu huu. (sun)

Everton haina mipango ya kumuuza mchezaji wa kiungo cha kati safu ya nyuma Mason Holgate msimu huu licha ya kuwa na nia ya kumnunua iliyoonyeshwa na timu ya West Brom, ambapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anacheza kwa deni. (Liverpool Echo)


Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri anaamini kuwa atafutwa kazi kabla ya msimu ujaona

Mchezaji wa safu ya mashambulizi wa Newcastle Muhispania Ayoze Perez, mwenye umri wa miaka 25, anasema klabu hiyo inapaswa kurefusha mkataba wa meneja Rafael Benitez , huku mazungumzo ya mkataba huo yakiwa yamesimamishwa hadi itakapoweza kuingia katika Ligi kuu ya Uingereza. (Chronicle)

Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri anaamini kuwa atafutwa kazi kabla ya msimu ujaona ameanza kupanga safari za Blues kabla ya kuanza kwa msimu. (Mirror)

Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amethibitisha kuwa klabu yake inamtaka mchezaji wa kati safu ya nyuma w Ajax na Uholanzi Matthijs de Ligt, mwenye umri wa miaka 19, baada ya kusiani mkataba na mchezaji mwenzake kwenye timu hiyo Frenkie de Jong, mwenye umri wa miaka 21. (SER, via Independent)

Liverpool wamefanya mazungumzo na RB Leipzig kwa ajili ya kusaini tmkataba na mshambuliaji huyo wa Ujerumani Timo Werner, mwenye umri wa miaka 23, msimu huu. (Bild, via Liverpool Echo)

Juventus wanaangalia uwezekano wa kuwaweka pamoja meneja wa zamani Antonio Conte na mchezaji wa zamani wa safu ya kati Andrea Pirlo kama msaidizi wake ikiwa meneja aliyepo sasa Massimiliano Allegri ataondoka kwenye klabu hiyo. (Tuttosport – in Italian)


Mchezaji wa zamani wa safu ya kati wa Juventus kushirikiana na Andrea Pirlo Meneja wa zamani wa Juventus Antonio Conte, ikiwa Massimiliano Allegri atahama

Leicester wanaweza kuiomba Monaco kumfanya Mreno Adrien Silva mwenye umri wa miaka 29 anayeicheziea kwa deni kuhamia huko kabisa ili kupunguza gharama ya pauni milioni arobaini (£40m)- ambayo ndiyo kiwango cha thamani ya mchezaji wa safu ya kati ya Ubelgiji Youri Tielemans, mwenye umri wa miaka 21, ambaye anacheza kwa deni katika Foxes nchini Ufaransa. (Leicester Mercury)

Meneja wa kikosi cha vijana cha Borussia Dortmund Lars Ricken anasema klabu hiyo itaendelea kuwalenga vijana wa Kiingereza baada ya kuhfanikiwa kusaini mkataba na winga wa England Jadon Sancho, R Kelly avunja ukimya mwenye umri wa miaka 18, kutoka Manchester City. (Evening Standard)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Chelsea Mfaransa Tiemoue Bakayoko, mwenye umri wa miaka 24, anasema kuwa hana uhakika juu ya hatua atakayoichukua baada ya kumalizika kwa msimu mrefu wa deni katika AC Milan . (France Football – in French)

Hull wameazimia kusaini mkataba na mlinda lango wa Reading Luke Southwood, mwenye umri wa miaka 21, ambaye ni mchezaji wa mkopo katika Ligi ya taifa kutoka Eastleigh. (Mail)

Chanzo BBC.

By Ally Juma.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents