TFF yawaondoa wachezaji wa Simba ndani ya ‘Taifa Stars’, viongozi wao kupelekwa kwa pilato
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limewaengua katika kikosi cha timu ya taifa ‘Taifa Stars’ wachezaji sita wa timu ya Simba kutokana na kuchelewa kuripoti kambini kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na kocha, Emmanuel Amunike.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao
Nyota hao walitakiwa kuripoti kambini jana usiku huku wakiwa wamepewa taarifa wakati Aishi Manula pekee ndiye aliyeripoti.
Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao amewaambia waandishi wa habari kuwa kocha Amunike amekasirishwa na kitendo hicho na kuamua kuchukua maamuzi hayo amabayo Shirikisho hilo chini ya Rais Wallace Karia wamelipitisha.
“Wachezaji wote wa Simba walioitwa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ isipokuwa Aishi Manula wameenguliwa katika kikosi kinachojiandaa na mchezo wa kufuzu dhidi ya Uganda kutokana na kutoripoti kambini kwa muda uliopangwa,” Wilfred Kidao Katibu Mkuu TFF.
Kidao ameongeza kuwa TFF iliamua kusogeza mbele mechi za Simba, Azam na Yanga zilipokuwa zichezwe Septemba mosi na pili ili kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Afrika dhidi ya Uganda ‘The Cranes’ utakaofanyika Septemba 8 jijini Kampala. “TFF imewaengua wachezaji sita wa Simba kwenye kikosi cha timu ya taifa kutokana na kuchelewa kuripoti kambini licha ya kupewa taarifa mapema,” alisema Kidao.
Wachezaji hao ni Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Hassan Dilunga, John Bocco na Shiza Kichuya.
Mbali na wachezaji hao viongozi wa Simba, Hamisi Kisiwa na meneja Richard Robert watapelekwa katika kamati ya maadili ya TFF siku ya Jumamosi ili kuchukuliwa hatua.
Uganda 5-0 Tanzania
watovu Wa Nidhamu Na simba Ipo kwenye Ubora sana Na kutokana a Hilo wachezaji Wao wameanza kujisikia Mbona aishi manula yeye Kazingatia maagizo ya Mwalimu Mnakosa Baraka kwa watz kisa Huo usimba na Uyanga Kuweni Wazalendo Lakini sio mbaya kuna vijana pia wameitwa mlipotoka Nyie Acha waonesha cheche..
5-0 mbn chache huyu Amonike anadhani Uganda niwakuchezea program yamaandali ilitakiwa kwa pamoja mechi trh 12 mchezaji kachelewa Siku moja unamuondoa wayanga nawaliopo nje hawajafika hiyo program unatengeneza kwa timu nusu angekuwa nasubra timu ikamilike kilalaheri Uganda na safari ya kocha kubakia Tanzania nindogo kama kaanza kwa mbwembwe
Francis Kimpa wakifanya hivyo mimi kuanzia leo mganda mpaka tuwafunge Tanzania ndo nachukua uraia wa Tanzania sioni chamana kitakacho fanyika
Labda hujui umuhimu wa hao wachezaji kwenye timu ya taifa…chezeni bila wao ndo utajua umuhimu wao kwenye kikosi
Uganda 4 Tz 0
Kocha amechukua maamuzi ya jaziba,kingine ambacho nakiona hapa wachezaji wamekosa morali ya kuichezea timu yao ya taifa,wanaona ni kitu cha kawaida kuna vitu vinatakiwa vifanyike waipende timu yao
Taifa stars haina wachezaji, wachezaji ni mali ya klabu, kuwaengua ni sawa kulingana na utaratibu wako ila uje na ushindi vinginevyo, utakuwa kwenye shinikizo zaidi ya mourintho
Hahahaaa
Kocha hawajui wabongo akifungwaa ndoatatujua vizur
Kocha kafanya cha maana sana kuwaondoa wakina simba maana simba wanajiona wenyewe ndo Tanzania kabsa hawajui kuwa ni nafas pekee wanayo kuwa wamependelewa kutoka ktk vilabu vitatu simba ,,,,yanga na azam ambapo kuna vilabu vingne vina tamani wachezaji wao kuwemo kwenye timu ya taifa na havimo mm naona tuna vilabu vingi sana hapa bonge hebu wapewe nafasi na vilabu vingne waonyeshe uwezo wao na wanaweza fanya vzr zaid ya hao wanaolinga linga
Tanzania amu elewi ata mû pira na amuwezi fika ata kwenyi robo final ata kidogo.
Chiku Mudy ngoja atafurahia shoo