Burudani
The CEO: Filamu inayofanyika kwenye nchi zaidi ya tano Afrika, bajeti yake ni dola milioni 1
Kwa miaka mingi filamu za Afrika zimekuwa zikitumia bajeti ndogo kutokana na uchumi.
Hata Nollywood ambao kiwanda chao kinadaiwa kuwa na thamani ya dola bilioni 4.3 au asilimia 1.2 la pato la taifa, bado imeendelea kuwa na filamu za kawaida.
Hata hivyo kuna filamu iliyopo kwenye hatua za utengenezaji iitwayo ‘The CEO’ inaweza kuja kuwa na tofauti kubwa.
Kwa mujibu wa muongozaji wa filamu hiyo, The CEO inakilisha bara zima.
Miongoni mwa waigizaji wa filamu hiyo ni muimbaji wa Benin na mshindi wa tuzo za Grammy, Angelique Kidjo. Waigizaji wengine wanatokea South Africa, Kenya, Ivory Coast na Morocco.