Michezo

Thierry Henry amkana Alexis Sanchez kwa hili

Thierry Henry kwa sasa amepachikwa majina mengi ya kejeli na mashabiki wa Arsenal kutokana na madai ya kumshawishi Alexis Sanchez kujiunga na Manchester United.

Wengine wamekuwa wakimuita nyoka msaliti na mengine mengi. Kocha huyo msaidizi wa timu ya taifa ya Ubelgiji na mchezaji wa zamani wa Arsenal amekana kuwa hakuwahi kumshauri Sanchez kufanya maamuzi hayo.

Henry ametoa taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa Twitter, ameandika, “Ninajua sihitaji kuelezea hili kwa mashabiki wengi wa Arsenal lakini kinyume na uvumi hakuna muda wowote nilimwambia Alexis Sanchez aondoke Arsenal. Sikujua kwamba angeenda kusajiliwa na Man Utd mpaka nilipoona kwenye habari kama wengine.”

Baada ya kukamilisha usajili wa kujiunga na Man United, Alexis Sanchez alithibitisha kwa kuandika ujumbe kuwa alipokea ushauri wa kuondoka Arsenal na kujiunga na Manchester kutoka kwa Henry.

“Nakumbuka leo, mazungumzo niliyokuwa nayo na Henry, mchezaji wa kihistoria wa Arsenal, ambaye alibadilisha klabu kwa sababu hiyo hiyo na leo ni wakati wangu,” aliandika Sanchez.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents