Michezo

Tiger Woods aanza kupatiwa msaada wa kitaalamu

Mchezaji golf maarufu duniani Tiger Woods, ambaye alikamatwa mwezi Mei katika jimbo la Florida kwa kosa la kuendesha gari huku akiwa amelewa amesema kuwa kwa sasa yupo chini ya uangalizi wa kupatiwa matibabu ya kitaalumu.

Mchezaji huyo ambaye alifunguliwa kesi kutokana na kosa hilo amesema kuwa kwa sasa anapata msaada huo ila sio kuwa yupo rehab.

“I’m currently receiving professional help to manage my medications and the ways that I deal with back pain and a sleep disorder,” amesema Woods.

Pia aliongeza kuwa “I want to thank everyone for the amazing outpouring of support and understanding especially the fans and players on tour.” Hata hivyo nyota huyo alikanusha kuwa hakuwa amelewa wakati polisi walipomkamata.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents