Habari

Tiketi za Kombe la dunia 2014 zagombaniwa ikiwa ni siku ya pili toka zianze kuuzwa

Mashabiki wa soka duniani walio na kiu ya kombe la dunia wameanza kuzikimbilia tiketi za kushuhudia mashindano hayo yatakayofanyika mwakani nchini Brazil.

brazil
Jumanne (August 20) tiketi za mashindano hayo makubwa duniani zilianza kuuzwa kupitia mtandao wa shirikisho la soka duniani FIFA na kwa mujibu wa BBC, FIFA imesema kuwa zaidi ya tiketi milioni moja zimeombwa kupitia mtandao wake ndani ya saa saba pekee tangu zianze kuuzwa.

Wengi walioagiza tiketi hizo ni mashabiki kutoka Brazil, Argentina, Marekani na Uingereza. Mechi za ufunguzi zitafanyika Alhamisi (June 12) na fainali itafanyika Jumapili (July 13) mwakani.

Mashabiki wa soka wanaweza kuomba tiketi hizo kupitia mtandao wa FIFA hadi tarehe kumi Oktoba.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents