Muziki
Tiko: Muigizaji mwingine wa kike aliyeingia kwenye muziki, sikiliza wimbo wake mpya
Anaitwa Tiko Hassan muigizaji wa filamu nchini ambaye mwaka huu ameamua kuingia studio za Mazuu Records na kufanya wimbo wake wa kwanza uitwao Watu. Kwa sasa yupo mbioni kumalizia albam yake ya kwanza ndani ya studio hizo.
Albam yake itakuwa na nyimbo zaidi ya 10 ambazo ni pamoja na Watu, Acha Love iyongee, Mimi na yeye na zingine. “Sijaacha maigizo bado nipo na muziki upo katika damu,” anasema mrembo huyo.