Mahojiano
Tommy Flavour amjibu Zuchu baada ya kuimba wimbo wake “Mimi shabiki wa Zuchu pia, mimi ni watoto wa kifalme (+Video)
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva aliyopo kwenye lebo ya Kings music inayosimamiw ana Alikiba Tommy Flavour amezungumzia kuhusu EP yake ambayo anatarajia kuiachia siku zijazo.
Mbali na hilo Tommy amezungumzia ngoma yake mpya ya THE ONE na kuwaomba mashabiki kuendelea kusapoti muziki wake na wasanii wote wa Bongo Fleva.
Tommy pia amemshukuru msanii kutoka lebo ya #WCB Zuchu na kuthibisha kuwa yeye ni shabiki namba moja wa muziki wa Zuchu huku akiitaja ngoma ya #Wana kama ngoma yake bora kutoka kwa msanii huyo.
“Wimbo wa Alikiba #Midiocre ni mkubwa sana kwanza nilishangaa kuona Alikiba amebadilika hivyo na hivyo mi nimependa kuona anabadilikabadilika”
https://www.youtube.com/watch?v=OYZE_3iYCjg