Treni ya kifahari zaidi duniani yawasili Tanzania na watalii 64 kutoka Ujerumani (+picha)
Watalii 64 kutoka nchini Ujerumani wamewasili Jijini Dar es Salaam leo Septemba 2, 2018 kupitia reli ya TAZARA wakitokea nchini Afrika ya Kusini kwa kutumia treni maarufu ya kitalii ijulikanayo kama ROVOS ya nchini humo.
Watalii hao wamekuja Tanzania kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali yenye vivutio vya utalii hapa nchini ikiwemo mbuga za wanyama na visiwa vya Zanzibar.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuwapokea watalii hao iliyofanyika stesheni ya TAZARA Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa TAZARA Tanzania, Fuad Abdallah alieleza kuwa treni hiyo iliondoka mji wa Cape Town nchini Afrika ya Kusini Agosti 18, mwaka huu.
βWatalii mbalimbali huja nchini mara tano kwa mwaka kwa kutumia ROVOS kupitia reli ya TAZARA na nchi yetu hunufaika na ujio huu hasa faida za kiuchumi,β amesema Fuad.
Aidha alibainisha kuwa treni ya ROVOS ni miongoni mwa treni tatu bora duniani, hivyo ujio wa treni hiyo na watalii unatokana na vivutio bora vya utalii na miundombinu mizuri ya reli ya TAZARA.
βTreni hii inatumia reli ya TAZARA kuleta watalii kwa sababu nchi yetu imekidhi vigezo vya utalii na reli yetu imekidhi vigezo vya usalama na mawasiliano ya uhakika,β aliongeza Fuad.
Alisema kuwa katika safari hiyo ya treni watalii hao pia walipata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Selous iliyopo kusini mwa Tanzania na kuona wanyama mbalimbali wanaopatikana kwenye hifadhi hiyo.
Wakizungumza kwa furaha ya kuwasili Tanzania, watalii hao wa kijerumani walisema kuwa wamefurahia sana safari hiyo na mapokezi mazuri ya watanzania na kuahidi kurudi kwa mara nyingine.
Kwa upande wake mfanyakazi wa treni ya ROVOS, Monica Rieder mwenye asili ya Ujerumani alisema kuwa amewahi kufika Tanzania mara 14 na anavutiwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo yanayofanyika hapa nchini siku hadi siku.
ROVOS inatajwa kuwa moja ya treni tatu bora zaidi za kifahari duniani ambazo zinajihusisha na kusafirisha watalii na makao yake makuu yapo nchini Afrika Kusini.
TAZARA ni shirika la reli ya pamoja ya Tanzania na Zambia iliyoanza mwaka 1976 na inamilikiwa kwa asilimia 50 kila upande.
Kwaio kuna tren kutoka Tanzania πΉπΏ mpaka German π©πͺ??? At Johannesburg south Africa πΏπ¦
ilibebwa kwenye meli au
Duuuuu imepakiwa kwenye ndege au loli
Kuna urakini hapo
Watalii wametoka Germany mpaka Tanzania na Trainπ³π
aiseee hakuna haja ya kupanda ndege tena,tren inatosha mpaka ulaya…….
imepita reli gani??
WaTanzania kwa sifa tu siwawezi. Hio treni kutoka Germany mpaka tz ππ halaf inawatalii ndaniπ π
Hahahahahaah ilikuwa inapaa nn
Reri ya matope
Hahahaaa sio #kweli kwani hyo #Reli ilijengwa lini
ilipitia wapijomba?
Huend labd ni tatizo la kutumia vibaya kiunganishi kati ya neno moja na jingine hio huweza leta maana tofaut.
Upo pnd ip nao?@Mnyara
Imepita kwenye reli gan??
rudi shule wewe
Alietafsiri lugha mungu anamuona
Angani ya umeme
Hahahaha soma habari nzima na sio kichwa cha habari tuu..ndo maana umekomenti utumbo wa panya
Ahahahahaha utangoja sana
Imetoka afrika kusin na tren hiyo mara kwa mara huja
Kwani ni bando au kutokuelewa kusoma manake i ao yesha aujasoma habari nzima,ila umesoma kichwa cha habari
Heheheheheheh wabongo nawagawa bure..amfungui habari na kuisoma zaidi ila mnatumia bando kukomenti uhozo haya mungu anawaona shauri yenu..
Leli ipo sema hao watarii wamepandia afrika kusin na hukuja mara kawa mara
Tazara
Khu
Kwa kupitia reli ipi?