Habari

Trump maji ya shingo, ajipa moyo kampeni yake ina kiki bado

​Mgombea wa urais kupitia chama cha Republican, Donald Trump amesisitiza kuwa kampeni yake imeshikamana licha ya ripoti kuwa kuna mpasuko mkubwa ndani ya chama chake kutokana na uropokaji mkubwa alioufanya.


Akihutubia huko Florida, Trump alisema kampeni yake inaendelea vyema.

Vyombo vya habari vya Marekani vimedai kuwa alisababisha kero kubwa alipowashambulia wazazi wa mwanajeshi wa Marekani aliyeuawa.

Baadhi ya wafanyakazi wa kampeni yake waliiambia CNN kuwa wanahisi kama wanapoteza muda wao.

“It’s never been so well united… I would say right now it’sthe best in terms of being united that it’s been since we began, ” aliwapa moyo wafuasi wake.

Trump anapambana na upinzani mkubwa kutoka kwa mgombea wa chama cha Republican, Hillary Clinton.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents