Habari
Tumesikitishwa sana, Diamond alichelewa masaa matatu kufika Airport Mwanza – ATCL
Kampuni ya ndege Tanzania (ATCL ) limetoa taarifa rasmi kuhusu sakata la Msanii wa muziki, Diamond Platnumz kuchelewa Airport Jijini Mwanza usiku wa jana.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Diamond alitakiwa kufika saa 11:45 jioni lakini yeye alifika saa 2:15 usiku. Ikiwa tayari ndege ilibakiza dakika 30 kuondoka kuelekea Dar Es Salaam .