Michezo

Tunaomba radhi – Saudi Arabia


Shirikisho la Soka la Saudi Arabia (SAFF), limeomba radhi kwa kusahau kuwa kimya kwa dakika kadhaa kama ishara ya kuomboleza shambulio la kigaidi lililotokea jijini London kabla ya mechi ya timu yao ya taifa dhidi ya Australia.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Australia wakiwa wametulia kwa muda kuomboleza shambulio la London

Taarifa iliyotolewa na (SAFF) ilisema, “Tunaomba radhi kwa kosa tulilotenda kutokana na wawakilishi wetu kusahau kukaa kimya kwa dakika kadhaa kuomboleza shambulio la London.”

Shirikisho la Soka la Saudi Arabia (SAFF)

Shambulio hilo lilitokea Juni 3 na kuua watu saba, huku wengine kadhaa wakijeruhiwa. Hilo ni tukio la pili wakati lingine lilitokea mwezi Mei.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Australia wakishangilia baada ya kufunga bao

Shirikisho hilo lilisema kwamba linapinga vikali vitendo vyote vya kigaidi na linaungana na wanafamilia wote wa walioathirika kwa namna moja ama nyingine nyingine.

Katika mchezo huo  Saudi Arabia walikubali kipigo cha magoli 3-2 ikiwa ni mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia hapo mwakani.

BY HAMZA FUMO

 

 

 

 

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents