Michezo

Tunautaka Ubingwa wa FA kama tulivofanya Ligi Kuu, atakayeshiriki Kimataifa tutampendekeza sisi -Mratibu wa Simba (+Video)

Mratibu wa klabu ya Simba Abbas Ally amesema Mnyama Simba anautaka Ubingwa wa FA pia na hawana mpango wa kukiacha kikombe na utakapofika muda wa nani kushiriki michezo ya Kimataifa wataituma Azam FC kwenda kushiriki kombe la Shiriko Barani Afrika.

Kwa mujibu wa kanuni za soka nchini, Bingwa wa kombe la Ligi Kuu ndiye anayepata nafasi ya kushiriki Kombe la Klabu bingwa Barani Afrika.

Na Bingwa wa FA ndiye anayeiwakilisha nchi katika Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Kwa sasa Simba SC ndiye bingwa wa Ligi Kuu na hivyo tayari anao uhakika wa kuiwakilisha nchi Kimataifa, Je kama Mnyama Simba akachukua na Kombe la FA nani ataiwakilisha nchi katika nchi kwenye kombe la Shirikisho ?

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents