Burudani
Tunda Man amshirikisha tena Alikiba kwenye ngoma mpya
Baada ya kumshirikisha kwenye Msambinungwa, Tunda Man anatarajia kumshirikisha tena Alikiba kwenye ngoma mpya iitwayo ‘Baby’.
Tunda ameiambia Bongo5 kuwa wakati anajiandaa kumalizia project yake ya ‘Achana na Mimi’ pia anajipanga kumalizia project hiyo na Alikiba.
“Nina project mpya na Kiba, ngoma inaitwa Baby,” amesema msanii huyo.
“Ni ngoma ambayo imemalizika bado tupo kwenye mipango ya video ndo tunaangalia mazingira, ila kila kitu kipo tayari kuhusu maandalizi. Kuna kazi nyingi na collabo zinakuja kwahiyo mashabiki wa muziki wangu wakae mkao wa kula.”