Habari
Tundu Lissu amaliza matibabu yake Ubelgiji, Ahofia kurudi Tanzania kisa ‘Watu wasiojulikana’ (+video)
Mwanasheria mkuu wa CHADEMA, Mhe. Tundu Lissu amesema kuwa kwa sasa amemaliza matibabu yake nchini Ubelgiji ila bado anahofu ya kurudi Tanzania.
Akiongea kwenye mahojiano yake na idhaa ya kiswahili ya VoA, Lissu amesema kwa sasa hana kisingizio cha matibabu kwani amemaliza matibabu ila anashindwa kurudi Tanzania kwa kuhofia usalama wake.
Lissu amesema watu wasiojulikana waliomshambulia miaka miwili iliyopita bado hawajakamatwa, Hivyo anasubiri hadi apate uhakika wa usalama wake.
https://www.instagram.com/tv/B3bL2ObhfzG/?igshid=1p5xy5ulsafgd