Habari

Twiga Bankcorp kuwasaka wadaiwa sugu

Benki ya Twiga Bankcorp imeanza msako wa wadaiwa sugu wa benki hiyo ambapo kiasi cha shilingi bilioni 8 hazijarejeshwa na wateja waliochukua mkopo katika benki hiyo ambayo kwasasa ipo chini ya usimamizi wa benki kuu ya Tanzania BOT. Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya benki hiyo kuanza tena kutoa baadhi ya huduma kwa wateja wake.

dsc_0736-1

Msako wa wadaiwa sugu wa benki Twiga Bankcorp umeanza rasmi jijini Dar es salaam, ukiwa chini ya kampuni ya ufilisi ya MARCAS. Msako huu umeanza katika maduka ya wadaiwa wa benki hiyo eneo la Segerea jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa kampuni ya Ufilisi ya MARCAS inayohusika na ukusanyaji wa madeni ya Twiga Benkcorp Richard Paul ameelezea lengo la msako huo.

“Zoezi hili ni endelevu, zoezi hili litafanyika Tanzania nzima kwa wale wote waliokopa ndani ya benki ya Twiga nakukimbia na hizo pesa za Twiga. Zoezi hili ni endelevu na litaanza hapa,tukafunga maduka Kariakoo,tukaenda mpaka kwenye nyumba za vigogo waliokopa hela benki na watu wote waliokopa hela benki tumewakamata,”alisema Paul.

Oktoba 28 mwaka huu, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu alitangaza benki hiyo kumilikiwa na kuchukua usimamizi na benki kuu ya Tanzania.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents