Fahamu

Twiga wafupi zaidi duniani wagunduliwa Afrika

Kikundi cha wanasayansi kimegundua aina mpya ya twiga ambao ni wafupi barani Afrika- twiga hawa wana kimo cha mara mbili cha twiga wa kawaida.

Twiga hao wawili kutoka maeneo mawili tofauti, mmoja alipatikana Namibia na mwingine Uganda.

Twiga hawa watawasilisha mfano wa twiga wafupi katika makala inayoandaliwa na taasisi ya hifadhi ya twiga.

Twiga hawa wana miguu mifupi zaidi ya twiga wengine.

Wanasayansi walibaini utofauti wao wakati wakipiga picha za utafiti wa idadi ya twiga waliopo Afrika.

“Inawezekana wana utofauti mwingine katika ukuaji,” alisema Michael Brown kutoka taasisi ya hifadhi ya twiga.

Alisema twiga hao wana zaidi ya mwaka .

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents