Twitter wauondoa ujumbe wa Trump uliokuwa unawatishia waandamanaji kwamba watapigwa risasi
Mtandao wa Twitter umeufuta ujumbe uliyotumwa na Rais Trump kwa madai unachochea vurugu.
Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi Minneapolis kuandamana kwa siku ya tatu kufuatia kifo na mtu mweusi George Floyd ambaye aliuwawa na polisi muda mchache baada ya kuwekwa chini ya ulinzi.
Ujumbe huo wa pili ambao aliuweka mtandaoni Alhamisi Asubuhi, ulisomeka “…These THUGS are dishonoring the memory of George Floyd, and I won’t let that happen. Just spoke to Governor Tim Walz and told him that the Military is with him all the way. Any difficulty and we will assume control but, when the looting starts, the shooting starts. Thank you
Chapisho hilo liliwekwa alama ya onyo ikisema inakiuka miongozo ya Twitter .
Hii inakuja baada ya kampuni hiyo kuongeza ukaguzi kwenye Twitter za rais Trump alisaini agizo kuu la kukagua sheria zinazolinda kampuni za vyombo vya habari.