Burudani

Ubaguzi wafanya Solange Knowles afute akaunti ya Twitter

Msanii wa muzuki Solange Knowles, ambaye ni mdogo wake na msanii Beyonce amefutilia mbali akaunti yake ya mtandao wa Twitter kwa kuonyesha kukerwa na mapigano yanayoendelea katika mji wa Charlottesville, uliopo Virginia- Marekani.

Msanii huyo aliandika ujumbe katika mtandao huo kabla ya kufuta kuonyesha yupo upande wa mwadada Takiya Thompson, aliyekamatwa kwa kuhusika kuweka mkutano wa adhara unaoonyesha ukipinga ubaguzi wa rangi mji huo.

“Deleting my twitter soon, but before I dip when we gonna pull up ? & what we got to do to get my new hero Takiyah Thompson free?,” ameandika Solange.

Hata hivyo msanii huyo hakuishia hapo akahamia katika mtandao wa Instagram kuonyesha kukerwa na mapigano yakiopo dhidi ya ubaguzi na kupelekea watu takribani 22 kufariki mpaka sasa.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents