Habari

Ubalozi wa Saudi Arabia waunga mkono jitihada za RC Makonda matababu ya moyo kwa watoto (Video)

Kampeni ya Matibabu ya Upasuaji wa Moyo Kwa watoto kutoka familia Duni iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda imezidi kuwa na mafanikio makubwa ambapo Balozi wa Saudi Arabia Nchini Tanzania MOHAMED BIN MANSOUR kupitia taasisi ya King Salman wameunga mkono jitiada hizo kwa kumpatia madaktari bingwa wa Moyo ambao hadi siku ya leo wamefanya upasuaji kwa Watoto 64 kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

https://www.instagram.com/p/B5urfx7h50I/

RC Makonda amemshukuru Balozi huyo kwa kuthamini uhai wa Watoto hao ambao waliteseka na kukata tamaa ya kuishi kutokana na Wazazi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu huku watoto wengine wakiwa ni yatima.

Aidha RC Makonda amesema kuwa Kampeni ya kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni moja kwaajili ya matibabu ya Moyo Kwa watoto zaidi ya 500 kutoka taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete inaendelea vizuri na hivi karibuni ataeleza hatua iliyofikiwa.

Pamoja na hayo RC Makonda amemuomba Balozi huyo wa Saudi Arabia na Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya kuangalia uwezekano wa Kupeleka kambi ya Matibabu ya Moyo Mkoani Mwanza ili iweze kuwahudumia Wananchi wa Kanda ya Ziwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwetwe Prof. Mohammed Janabi ameeleza kuwa upasuaji wa watoto hao 64 umeokoa kiasi cha Shilingi Milioni 465 ambazo wazazi wangepaswa kutoa lakini kupitia diplomasia nzuri kati ya Tanzania na Saudi Arabia watoto wao wamefanyiwa upasuaji bure.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents