Michezo
Uchambuzi: Mnyama Simba aunguruma, makosa manne ya Biashara (+Video)
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Simba SC wamefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa jumla ya magoli 4 – 0 dhidi ya Biashara United mchezo uliyopigwa katika dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia ushindi huo mnono @abbas__pira amekimwagia sifa lukuki kikosi cha Wekundu wa Msimbazi ambao kimeibebesha kapu la magoli timu ya Biashara United.