Burudani
UDSM kusaka vipaji kwenye tamasha la ‘The Talent Fever’
Wanafunzi wa Idara ya Sanaa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wameandaa tamasha la kusaka vipaji lililopewa jina ‘The Talent Fever.’
Tamasha hilo litafanyika Ijumaa ya April 21 katika idara ya sanaa katika chuo hicho.
Maonyesho ya sanaa za uchoraji na uchongaji yatafanyika kuanzia saa sita mchana mpaka 12 jioni ambapo maonesho mengine kama Live Music, Dancing, Stand-up Comedy (vichekesho), fashion show, Poetry (Ushairi), Stage Plays (maonyesho ya jukwaani) na mitindo huru ya hip hop yatafuatia.