Michezo

UEFA Champions League: Safari ya Man United kuelekea 16 bora yabaki njia panda

Jana usiku kulikuwa na michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya ambapo kulikuwa na michezo nane kwenye viwanja mbalimbali barani humo.

Kwenye mchezo uliovutia watu wengi ni ule wa Manchester United dhidi ya FC Basel ambapo klabu hiyo ilihitaji alama moja kufuzu hatua ya 16 bora. Lakini mambo hayakuwa hivyo kwani kunako dakika 89 vijana hao wa Basel walipata goli lililokwamishwa ndoto za vijana wa Mourinho kusonga mbele.

Kwa sasa Manchester United watahitaji pointi moja tu kufuzu kuingia 16 bora na endapo Man United watapoteza mchezo wao wa mwisho dhidi ya CSKA Moscow, Klabu ya Basel itatakiwa ishinde magoli angalau matano dhidi ya  na klabu ya Benfica.

Na klabu ya Moscow itahitaji ushindi wa goli nyingi dhidi ya Manchester United ili iweze kujihakikishia nafasi ya kufuzu.

Timu tatu kwenye ‘Kundi A’ yaani Manchester United, FC Basel na CSKA Moscow mpaka sasa bado zina nafasi ya kufuzu kuingia 16 Bora ya michuano hiyo ambapo ni timu mbili tu zinatakiwa kufuzu kwenye kila kundi.

Matokeo ya mechi nyingine ni kama ifuatavyo.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents