Michezo

UEFA wamtangaza refa atakayechezesha fainali ya Madrid na Liverpool

Mchezo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka duniani kwa sasa ni fainali ya klabu bingwa barani Ulaya ambayo itawakutanisha Real Madrid na Liverpool Jumamosi ya Mei 26 mwaka huu.

Tayari kamati ya waamuzi ya UEFA imemchagua mwamuzi wa kati ambaye anachezesha mchezo huo utakaopigwa kwenye uwanja wa NSC Olimpiyskiy, Kyiv kwa kusimamia sheria 17 za soka.

Kamati hiyo imemteua Milorad Mažić kutoka nchini Serbia kuchezesha fainali hiyo ambayo inataajiwa kuwa na upinzani mkubwa kwa timu zote mbili.

Mažić, 45, amekuwa mwamuzi wa kimataifa tangu 2009 na amewahi kuchezsha fainali kadhaa ikiwemo ile ya mabara mwaka jana iliyowakutanisha Chile and Germany, UEFA Super Cup 2016 kati ya Real Madrid na Sevilla.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents