Michezo

UEFAChampionsLeague: Harry Kane aiangamiza Borussia Dortmund (+Video)

Klabu ya Borussia Dortmund kutoka Ujerumani, jana imechabangwa goli 3-1 dhidi ya Tottenham Hotspur, kwenye mchezo wa klabu bingwa barani Ulaya.

https://youtu.be/nyW_nDVsBUA

Aliyeanza kufungua akaunti ya magoli ya Spurs ni Mkorea Heung-Min Son, kunako dakika 4′ kabla ya Mshambuliaji mwimba wa klabu hiyo, Harry Kane kutupia goli mbili kunako dakika ya 15′ na 60′ ya kipindi cha pili.

Borussia Dortmund hao walipata goli moja la kufutia machozi kupitia kwa Andriy Yarmolenko kunako 11 kipindi cha kwanza.

SOMA ZAIDI – UEFAChampionsLeague: Real Madrid waendeleza ubabe Ulaya (+Video)

Kwenye msimamo wa Kundi H, Spurs wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 3 sawa na vinara wa kundi hilo Real Madrid kukiwa ni tofauti ya magoli.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents