Michezo

UEFAChampionsLeague: Liverpool wavutwa shati na Sevilla (+video)

Klabu ya Liverpool kutoka Uingereza jana usiku imelazimishwa sare ya goli 2-2, na klabu ya Sevilla kutoka Hispania, Kwenye michuano ya kombe la klabu bingwa barani Ulaya.

https://youtu.be/sR7l17FxMd8

Sevilla ndio walikuwa wa kwanza kuliona lango la Liverpool kunako dakika ya 5 kipindi cha kwanza kupitia kwa, Wissam Ben Yedder kabla ya Mohammed Salah na Firmino kuongeza goli la pili na mpaka mapumziko ilikuwa 2-1.

Kipindi cha pili timu zote zilirudi kwa kasi lakini bahati haikuwa kwa Liverpool kwami mnamo dakika ya 72, mshambuliaji wa Sevilla, Joaquin Correa aliisawazishia Sevilla, mpaka dakika 90 ubao ulisomeka 2-2.

Matokeo mengine kwenye ya Kundi E, Maribor nao walilazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Spartak Moscow, matokeo ambayo yanafanya kundi hilo kila timu kuwa na alama 1.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents